Mamlaka ya bandari jijjni Dar es Salaam imetoa mchango wa vitanda 15 vya kuhudumia kina mama wajawazito katika hospitali ya rufaa ya Temeke Dar es Salaam.
Kufuatia msaada huo serikali iliyowakilishwa na mkuu wa wilaya ya Temeke, Mwanahamisi Mukunda imesema itaendelea kushirikiana na wadau na taasisi mbalimbali katika kuboresha miundombinu ya sekta ya afya ili kutoa fursa ya kuongeza ubora na ufanisi wa huduma katika hospitali zote nchini.
#AzamTVUpdates #AzamNews #TemekeReferralHospital #tpa #bandaridsm